Mapema leo Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Strong Women Foundation Neema Ng'asha,amefanikiwa kumpa Mtaji wa biashara ndogo mama anayepitia mazingira magumu,jijini Mwanza.
Neema Ng'asha ameiomba jamii kuwawezesha wanawake wenye moyo wa kufanya biashara ndogo ndogo kwa kuwapa mitaji ili waweze kujikwamua kiuchumi.
Pia ameomba wanawake kufanya kazi kwa bidii na kuomba msaada kwa wadau wawawezeshe pale wanapokwama kutimiza malengo yao.
Ni muhimu pia wanawake kujiunga katika vikundi na kujifunza kazi mbalimbali za ujasiriamali ili kujikwamua kiuchumi na wasiwasi tegemezi.

No comments:
Post a Comment