Kwa mawasiliano zaidi.
Tuesday, May 30, 2023
Strong Women Foundation(SWF) yaongea na watoto wa kike kusoma kwa bidii ili waweze kutimiza ndoto zao.
Meya wa jiji la Mwanza awa mgeni rasmi katika uzinduzi wa shirika la Strong Women Foundation (SWF)
Meya wa jiji la Mwanza,Mheshimiwa Sima Costantine Sima,amekuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa Shirika la Strong Women Foundation (SWF)lililopo jijini Mwanza.
( Mhe.Sima Costantine Sima akiongea)
Uzinduzi huu uliofanyika katika kumbuka wa Mwanza Hotel na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali wa maendeleo jijini Mwanza
Shirika la Strong Women Foundation ni asasi isiyokuwa ya kiserikali yenye makao yake makuu jijini Mwanza.Shirika hili linafanya kazi ya kusaidia wanawake,mabinti na watoto wanaopitia mazingira magumu.
(Bodi member wa Strong Women FoundationBeth Mpuya Gambaloya )Katika uzinduzi huu Meya wa jiji la Mwanza Amepongeza Mkurugenzi Mtendaji wa Strong Women Foundation Neema Ng'asha pamoja na viongozi wote wa shirika hilo kwa kazi njema wanayofanya kusaidia jamii yetu.
Kikundi cha MWANAMKE NGUZO kutoka Strong Women Foundation wakimuuzia mgeni rasmi bidhaa walizotengeneza.
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Strong Women Foundation atoa mtaji kwa mama anayepitia mazingira magumu
Mapema leo Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Strong Women Foundation Neema Ng'asha,amefanikiwa kumpa Mtaji wa biashara ndogo mama anayepitia mazingira magumu,jijini Mwanza.
Neema Ng'asha ameiomba jamii kuwawezesha wanawake wenye moyo wa kufanya biashara ndogo ndogo kwa kuwapa mitaji ili waweze kujikwamua kiuchumi.
Pia ameomba wanawake kufanya kazi kwa bidii na kuomba msaada kwa wadau wawawezeshe pale wanapokwama kutimiza malengo yao.
Ni muhimu pia wanawake kujiunga katika vikundi na kujifunza kazi mbalimbali za ujasiriamali ili kujikwamua kiuchumi na wasiwasi tegemezi.
Mkurugenzi Mtendaji wa Strong Women Foundation apeleka msaada wa chakula kwa watoto wanaoishi mazingira magumu
Shikira la Strong Women Foundation latoa msaada wa vifaa vya shule kwa watoto.
Shirika la Strong Women Foundation (SWF) Tanzania lenye makao yake makuu jijini Mwanza.Limetoa vifaa vya shule kwa watoto wanaopitia mazing...
-
Mkurugenzi mtendaji wa Strong Women Foundation,lililopo jijini Mwanza Neema Ng'asha,leo amekwenda kuwapa msaada wa chakula watoto wanao...
-
Muimbaji wa nyimbo za Injili kutoka jijini Mwanza Neema Ng'asha ameibuka kuwa mshindi wa Tuzo za Muimbaji bora wa nyimbo za injili kanda...
-
Mapema leo Strong Women Foundation (SWF) walitembelea shule ya msingi Mkolani,iliyopo jijini Mwanza kuongea na watoto wa kike. Strong Women...











